Isma kiduku ULINIDANGANYA ni story ya kweli
Ukizungumzia wasanii wanaokuja kwa kasi kunako game ya bongo fleva uwezi ukaliacha jina la ISMA KIDUKU kijana anaesumbua na wimbo wake mpya wa ULINIDANGANYA, Ukiskiliza kwa umakini mashahiri yaliyomo ndani huo wimbo wa ulinidanganya na kama ulishawahi kutendwa na mpenzi wako utajikuta unamwaga machozi bila kupigwa sababu ni wimbo ambao umeimbwa kwa hisia sana, NINI chanzo kilichopelekea Isma kiduku kuandika wimbo huu.. Kwenye mahojiano mafupi na msanii huyo Alitupa siri fupi iliyofanya kuandika mashahiri hayo yanayowatoa mchozi waliotendwa ""Kwenye maisha yangu alitokea mschana mmoja [jina kapuni] ambae alinifanya niamini kuwa hakuna kitu kutendwa katika maisha ya mapenzi aliniaminisha sana kwa mapenzi matamu maneno matamu mpaka pesa alinipa pindi nilipofulia, ilinifanya nikadharau mpaka baadhi maneno ya mamaangu kwa sababu yake, nilidumu nae miaka minne nilimuheshimu sana yeye na familia yake mamaake dadazake hata wadogo zake niliwaheshimu kwa kujua siku moja ningefunga n